(ABNA24.com) Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa utulivu na usalama ni vitu vilivyoshikamana barabara na kusisitiza kuwa Tehran inataka utawale moyo wa udugu, misimamo ya wastani, hekima na muono wa mbali katika uhusiano wa nchi za Asia Magharibi.
Rais Hassan Rouhani amesema hayo mjini Doushanbe, Tajikistan, alipoonana na Amir wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamad Aal Thani pambizoni mwa Mkutano wa Tano wa Kongamano la Maingiliano na Hatua za Kujenga Imani Barani Asia (CICA) na kuongeza kuwa, mashauriano ya pande mbili na ya pande kadhaa pamoja na kuweko ushirikiano zaidi baina ya nchi za eneo hili ndiyo njia pekee ya kupunguza hitilafu na kutatua matatizo ya eneo hili na kwamba daima Iran iko tayari kutoa ushirikiano unaotakiwa katika masuala yote.
Aidha amesema, uhusiano wa Iran na nchi jirani na rafiki hasa Qatar ni katika masuala yanayopewa kipaumbele kikubwa na siasa za nje za Jamhuri ya Kiislamu na kusisitiza kuwa, ulimwengu wa Kiislamu unahitajia umoja na mshikamano na bila ya shaka yoyote Tehran na Doha zinaweza kuwa na uhusiano mpana na mkubwa sana baina yao.
Vile vile amesema, uhusiano wa Iran na Qatar ni wa kidubu, kirafiki na wenye manufaa kwa watu wote wa eneo hili na bado kuna uwanda mpana wa kuweza kupanua wigo wa ushirikiano wa nchi hizi mbili ndugu hasa katika upande wa kiuchumi.
Kwa upande wake Amir wa Qatar, Sheikh Tami bin Hamad Aal Thani amesema, utatuzi wa hitilafu zote zilizopo kwenye eneo hili ni mazungumzo, ushirikiano baina ya nchi zote na njia za kisiasa zisizo za kijeshi. Amesema, nchi yake pia ina hamu ya kuimarisha zaidi na zaidi uhusiano wake na Iran katika nyuga zote.
/129
16 Yuni 2019 - 10:00
Lambar labari: 951516
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa utulivu na usalama ni vitu vilivyoshikamana barabara na kusisitiza kuwa Tehran inataka utawale moyo wa udugu, misimamo ya wastani, hekima na muono wa mbali katika uhusiano wa nchi za Asia Magharibi.